Thursday, November 26, 2009

"NDANI YA NYUMBA"NAKO II NAKO


Sijawahi kupata nafasi ya kufanya nao mahojiano ili kujua kwa kina maana au chanzo cha jina Nako 2 Nako.Pamoja na hayo,wengi wanawakubali na kwa mambo mbalimbali,yakiwemo binafsi,wameshagonga vichwa vya habari mara kwa mara. Walianzia A-Town/City kabla ya kuweka kambi jijini Dar.

Hivi karibuni wamefyatua kitu kipya.Wimbo unaitwa Ndani ya Nyumba ambao kutokana na Producer wake,Hermy B(kutoka B’Hitz Music) ni wimbo wa kustarehesha zaidi kuliko kuelimisha au vitu kama hivyo.

Kitu ambacho kimekuwa kikinivutia kutoka Nako2Nako ni aina yao ya kughani.Ina utofauti fulani hivi ambao kimsingi ni muhimu.Nimewahi kusisitiza katika “kijiwe” fulani kwamba kama mtu anataka kupata mafanikio fulani katika chochote anachotaka kukifanya,ni muhimu akawa “mbunifu”.Kwenye muziki hali ni hiyo hiyo.Lazima utoke tofauti.La sivyo,watu watakusikiliza na kukuacha solemba haraka iwezekanavyo.Huna jipya.

Wasikilize Nako2Nako katika Ndani ya Nyumba

No comments:

Post a Comment